Pages

TUNAJIUSISHA NA HABARI ZA AINA ZOTE NDANI NA NJE YA BONGO VILEVILE TUNAKODISHA VYOMBO VYA MUZIKI NA P.A MAENEO YOTE YA JIJI LA MWANZA NA NJE YA JIJI LA MWANZA KARIBUNI SANA

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI..:KIJANA AUAWA KWA KUCHOMWA MOTO HUKO MWANZA BAADA YA KUTUHUMIWA KUIBA PIKIPIKI....

Mtu mmoja anaesadikiwa kuwa ni jambazi ambaye hakufahamika jina anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 25 ameuwawa kwa kupigwa mawe kisha kuchomwa moto na mwingine kunusurika kuuwawa. Tukio hilo limetokea jana alfajiri katika kijiji cha Shibula kata ya Bugongwa wilayani Ilemela Mkoani Mwanza kufuatia tukio la wizi lilotokea usiku wa kuamkia jana katika mtaa wa Nyamwilolelwa ambapo pikipiki moja na paneli ya solar ziliibiwa. Katibu wa Sungusungu katika kijiji cha Shibula John Mashalia amesema kuwa kufuatia tukio hilo waliamua kuweka ulinzi shirikishi kuzunguka vijiji vyote na ndipo walipokutana na kijana huyo aliyeuwawa akiwa na kijana mwingine aliyefahamika kwa jina la Edward Aloyce ambao walidai wanatafuta pikipiki iliyopotea. Mashalia ameongeza kuwa kata ya Bugongwa imekuwa na matukio ya ujambazi mara kwa mara ikiwa ni pamoja na vitendo vya ubakaji kwa watoto na wanawake. Kwa upande wake mkaguzi msaidizi wa jeshi la polisi Joyce Kotecha amewataka wananchi wa kata hiyo kuacha kujichulia sheria mkononi na kwamba wawasiliane na uongozi wa kata yanapotokea matatizo ya namna hiyo.
Kijana aliyeuawa kwa kuchomwa moto
Vijana wa sungusungu wakiwa katika mlango wa duka ambapo kijana mwingine aliyenusurika alifungiwa kungoja polisi waje
Hii ni pikipiki ambayo vijana hao walienda nayo eneo la tukio
Polisi wakipanga jinsi ya kumtoa mtuhumiwa huyo
Ambulance ikiandaliwa kupakia maiti ya kijana huyo....
Polisi wakikagua makoti ambayo kijana aliyenusurika alikuwa ameyavaa
Kijana aliyenusurika aitwaye Mangi akitolewa ndani ya duka kwa ulinzi mkali na kupakiwa kwenye gari...
 

Kijana Mangi akiwa ndani ya gari, pembeni yake ni maiti ya mwenzake....

0 comments:

Chapisha Maoni