Aunt Ezekiel.
STAA
wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel amejikuta katika wakati mgumu baada
ya kuanguka ghafla kwa presha akiwa ‘location’ jijini Tanga, Risasi
Jumamosi lina habari hii.Kwa mujibu wa chanzo, Aunt akiwa katika harakati za kuigiza filamu anayocheza na Amri Athuman ‘Mzee Majuto’, ghafla alianguka na kukimbizwa katika Hospitali ya Gesha jijini humo.
Aunt Ezekiel akiwa hospitali amelazwa.Baada ya kuzipata habari hizi, mapaparazi wetu walimtafuta Aunt kwa njia ya simu na alipopatikana alikiri kuanguka kutokana na kusumbuliwa na presha ya kushuka.
“Kweli nilikuwa shutting na Mzee Majuto, ghafla nilianguka na kukimbizwa hospitali, wameniwekea dripu mkononi ila namshukuru Mungu, naendelea vizuri,” alisema Aunt.
0 comments:
Chapisha Maoni